Zaburi 105:23-36 NEN

Zaburi 105:23-36

105:23 Mdo 7:15; 13:17; Mwa 46:6; 47:28; Za 78:51Kisha Israeli akaingia Misri,

Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.

105:24 Kut 1:7; Kum 26:7; Mdo 7:17Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana,

akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,

105:25 Kut 4:21; 1:6-10; Mdo 7:19ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake,

wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.

105:26 Kut 3:10; 4:16; Hes 33:1; 16:5; 17:5-8Akamtuma Mose mtumishi wake,

pamoja na Aroni, aliyemchagua.

105:27 Za 105:28-37; Kut 7:8; 12:51; 4:17; 10:1; 3:20; Dan 4:3Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao,

miujiza yake katika nchi ya Hamu.

105:28 Mwa 1:4; Za 99:7; Kut 10:22; 7:22Alituma giza na nchi ikajaa giza,

kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?

105:29 Za 78:44; Kut 7:21Aligeuza maji yao kuwa damu,

ikasababisha samaki wao kufa.

105:30 Kut 8:2, 6Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia

hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.

105:31 Za 78:45; 107:25; 148:8; Kut 8:16-18; 8:21-24Alisema, yakaja makundi ya mainzi,

na viroboto katika nchi yao yote.

105:32 Kut 9:22-25; Ay 38:22; Za 78:47Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe,

yenye umeme wa radi nchini yao yote,

105:33 Za 78:47; Kut 10:5, 12akaharibu mizabibu yao na miti ya tini,

na akaangamiza miti ya nchi yao.

105:34 Za 107:25; Kut 10:4, 12-15; 1Fal 8:27; Yoe 1:6Alisema, nzige wakaja,

tunutu wasio na idadi,

wakala kila jani katika nchi yao,

wakala mazao ya ardhi yao.

105:36 Kut 4:23; 12:12Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao,

matunda ya kwanza ya ujana wao wote.

Read More of Zaburi 105