Zaburi 105:12-22 NEN

Zaburi 105:12-22

105:12 Kum 7:7; Ebr 11:9; Mwa 17:8; 23:4; 34:30Walipokuwa wachache kwa idadi,

wachache sana na wageni ndani yake,

105:13 Mwa 15:13-16; Hes 32:13; 33:3-49walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine,

kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.

105:14 Mwa 35:5; 12:17-20; 20:3; Za 9:5Hakuruhusu mtu yeyote awaonee;

kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:

105:15 Mwa 26:11; 20:7; 1Sam 12:3“Msiwaguse niliowatia mafuta;

msiwadhuru manabii wangu.”

105:16 Isa 3:1; Law 26:26; Mwa 12:10; 41:54; 2Fal 8:1; Eze 4:16Akaiita njaa juu ya nchi

na kuharibu chakula chao chote,

105:17 Mwa 45:5; 37:28; Mdo 7:9naye akatuma mtu mbele yao,

Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.

105:18 Mwa 40:15Walichubua miguu yake kwa minyororo,

shingo yake ilifungwa kwa chuma,

105:19 Mwa 12:10; 41:40; 40:20-21hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia,

hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.

105:20 Mwa 41:14Mfalme alituma watu wakamfungua,

mtawala wa watu alimwachia huru.

Alimfanya mkuu wa nyumba yake,

mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,

105:22 Mwa 41:43-44; 41:40kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo

na kuwafundisha wazee wake hekima.

Read More of Zaburi 105