Zaburi 105:1-11 NEN

Zaburi 105:1-11

Zaburi 105

Uaminifu Wa Mungu Kwa Israeli

(1 Nyakati 16:8-22)

105:1 1Nya 16:34; Za 80:18; 99:6; 116:13; Yoe 2:32; Mdo 2:21; Isa 12:4Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake,

wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.

105:2 Za 30:4; 146:2; 33:3; 96:1; 7:17; 18:49; 27:6; 59:17; 71:22; 75:1Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa,

waambieni matendo yake yote ya ajabu.

105:3 Za 89:16Lishangilieni jina lake takatifu,

mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.

105:4 Za 24:6; 27:8Mtafuteni Bwana na nguvu zake,

utafuteni uso wake siku zote.

105:5 Za 40:5; Kum 7:18; 8:2Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya,

miujiza yake na hukumu alizozitamka,

105:6 Za 105:42; Kum 10:15; Za 106:5enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake,

enyi wana wa Yakobo, wateule wake.

105:7 Isa 26:8Yeye ndiye Bwana Mungu wetu,

hukumu zake zimo duniani pote.

105:8 Mwa 9:15; Za 106:45; 111:5; Eze 16:60; Lk 1:72Hulikumbuka agano lake milele,

neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,

105:9 Mwa 22:16-18; 15:18; Ebr 6:17; Lk 1:73; 17:2; 12:7; Gal 3:15-18; Dan 9:4agano alilolifanya na Abrahamu,

kiapo alichomwapia Isaki.

105:10 Mwa 28:13-15; Isa 55:3Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri,

kwa Israeli liwe agano la milele:

105:11 Mwa 12:7; Hes 34:2“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani

kuwa sehemu utakayoirithi.”

Read More of Zaburi 105