Zaburi 104:19-30 NEN

Zaburi 104:19-30

104:19 Mwa 1:14; Za 19:6; Ay 38:12Mwezi hugawanya majira,

na jua hutambua wakati wake wa kutua.

104:20 Isa 45:7; Amo 5:8; Za 74:16; 50:10Unaleta giza, kunakuwa usiku,

wanyama wote wa mwituni huzurura.

104:21 Amo 3:4; Za 145:15; Mt 6:26; Yoe 1:20Simba hunguruma kwa mawindo yao,

na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.

104:22 Za 37:8Jua huchomoza, nao huondoka,

hurudi na kulala katika mapango yao.

104:23 Mwa 3:19; Amu 19:16Kisha mwanadamu huenda kazini mwake,

katika kazi yake mpaka jioni.

104:24 Mwa 1:31; 1:20-22; Za 40:5; 24:1; 50:10, 11Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi!

Kwa hekima ulizifanya zote,

dunia imejaa viumbe vyako.

104:25 Za 69:34; Eze 47:10Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele,

imejaa viumbe visivyo na idadi,

vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.

104:26 Za 107:23; Eze 27:9; Yon 1:3; Ay 41:1; 40:20; Mwa 1:21Huko meli huenda na kurudi,

pia Lewiathani,104:26 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. uliyemuumba acheze ndani yake.

104:27 Ay 36:31; Za 147:9; 145:15; Rum 11:36Hawa wote wanakutazamia wewe,

uwape chakula chao kwa wakati wake.

104:28 Isa 58:11; Za 103:5; 145:16Wakati unapowapa,

wanakikusanya,

unapofumbua mkono wako,

wao wanashibishwa mema.

104:29 Kum 31:17; Ay 7:21; Mhu 12:7Unapoficha uso wako,

wanapata hofu,

unapoondoa pumzi yao,

wanakufa na kurudi mavumbini.

104:30 Mwa 1:2; Isa 32:15Unapopeleka Roho wako,

wanaumbwa,

nawe huufanya upya uso wa dunia.

Read More of Zaburi 104