Zaburi 104:19-30
104:19 Mwa 1:14; Za 19:6; Ay 38:12Mwezi hugawanya majira,
na jua hutambua wakati wake wa kutua.
104:20 Isa 45:7; Amo 5:8; Za 74:16; 50:10Unaleta giza, kunakuwa usiku,
wanyama wote wa mwituni huzurura.
104:21 Amo 3:4; Za 145:15; Mt 6:26; Yoe 1:20Simba hunguruma kwa mawindo yao,
na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
104:22 Za 37:8Jua huchomoza, nao huondoka,
hurudi na kulala katika mapango yao.
104:23 Mwa 3:19; Amu 19:16Kisha mwanadamu huenda kazini mwake,
katika kazi yake mpaka jioni.
104:24 Mwa 1:31; 1:20-22; Za 40:5; 24:1; 50:10, 11Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi!
Kwa hekima ulizifanya zote,
dunia imejaa viumbe vyako.
104:25 Za 69:34; Eze 47:10Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele,
imejaa viumbe visivyo na idadi,
vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
104:26 Za 107:23; Eze 27:9; Yon 1:3; Ay 41:1; 40:20; Mwa 1:21Huko meli huenda na kurudi,
pia Lewiathani,104:26 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. uliyemuumba acheze ndani yake.
104:27 Ay 36:31; Za 147:9; 145:15; Rum 11:36Hawa wote wanakutazamia wewe,
uwape chakula chao kwa wakati wake.
104:28 Isa 58:11; Za 103:5; 145:16Wakati unapowapa,
wanakikusanya,
unapofumbua mkono wako,
wao wanashibishwa mema.
104:29 Kum 31:17; Ay 7:21; Mhu 12:7Unapoficha uso wako,
wanapata hofu,
unapoondoa pumzi yao,
wanakufa na kurudi mavumbini.
104:30 Mwa 1:2; Isa 32:15Unapopeleka Roho wako,
wanaumbwa,
nawe huufanya upya uso wa dunia.