Zaburi 103:13-22
103:13 Mal 3:17; Kum 8:5; 1Yn 3:1; Isa 63:15, 16Kama baba alivyo na huruma kwa watoto wake,
ndivyo Bwana anavyowahurumia wale wanaomcha;
103:14 Za 119:73; 139:13-15; 146:4; Isa 29:16; Mwa 2:7kwa kuwa anajua tulivyoumbwa,
anakumbuka kwamba sisi tu mavumbi.
103:15 Za 37:2; 90:5; 102:11; Yak 1:10; Isa 40:6; Ay 14:2Kuhusu mwanadamu, siku zake ni kama majani,
anachanua kama ua la shambani;
103:16 Isa 40:7; Hag 1:9; Ay 7:8upepo huvuma juu yake nalo hutoweka,
mahali pake hapalikumbuki tena.
103:17 Mwa 48:11; Ezr 9:12; Kut 20:6Lakini kutoka milele hata milele
upendo wa Bwana uko kwa wale wamchao,
nayo haki yake kwa watoto wa watoto wao:
103:18 Yn 14:15; Kum 7:9; 28:9; Za 119:52; Hes 15:40; Za 47:8; 80:1; 113:5; 22:28; 66:7; Dan 4:17kwa wale walishikao agano lake
na kukumbuka kuyatii mausia yake.
Bwana ameweka imara kiti chake cha enzi mbinguni,
ufalme wake unatawala juu ya vyote.
103:20 Neh 9:6; Lk 2:13; Ebr 1:14; Za 29:1; 28:6; 107:25; 135:7; 148:8; Mt 6:10Mhimidini Bwana, enyi malaika zake,
ninyi mlio mashujaa mnaozitii amri zake,
ninyi mnaotii neno lake.
103:21 1Fal 22:19; Neh 7:73; Dan 7:9; Mwa 32:2Mhimidini Bwana, ninyi jeshi lake lote la mbinguni,
ninyi watumishi wake mnaofanya mapenzi yake.
103:22 Za 104:1; 67:3; 19:1; 145:10; 150:1, 6Mhimidini Bwana, kazi zake zote
kila mahali katika milki yake.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.