Zaburi 102:12-17
102:12 Kut 15:18; 3:15; Isa 55:13; 63:12; 40:2; Za 135:13Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele,
sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
102:13 Za 119:126; 44:26; 77:7; Kum 32:36; 1Fal 3:26; Isa 54:8; 60:10; 40:2; Zek 10:6; Kut 13:10; Dan 8:19; Mdo 1:7Utainuka na kuihurumia Sayuni,
kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema;
wakati uliokubalika umewadia.
102:14 Dan 9:2Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako,
vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
102:15 1Fal 8:43; Isa 2:2; Za 67:7; 76:12; 138:4; 148:11Mataifa wataogopa jina la Bwana,
wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
102:16 Za 51:18; 8:1; Isa 60:1, 2Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni
na kutokea katika utukufu wake.
102:17 Neh 2:8; 1Fal 8:29; Za 4:1; 6:9Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,
wala hatadharau hoja yao.