Zaburi 10:12-18
10:12 Za 3:7; 9:12, 13; 17:7; 20:6; 106:26; Isa 26:11; Mik 5:9Inuka Bwana! Inua mkono wako, Ee Mungu.
Usiwasahau wanyonge.
10:13 Ay 31:14Kwa nini mtu mwovu anamtukana Mungu?
Kwa nini anajiambia mwenyewe,
“Hataniita nitoe hesabu?”
10:14 Za 22:11; 37:5; Kum 33:29Lakini wewe, Ee Mungu, unaona shida na huzuni,
umekubali kuyapokea mkononi mwako.
Mhanga anajisalimisha kwako,
wewe ni msaada wa yatima.
10:15 Ay 31:22Vunja mkono wa mtu mwovu na mbaya,
mwite atoe hesabu ya maovu yake
ambayo yasingejulikana.
10:16 Kut 15:18; Kum 8:20Bwana ni Mfalme milele na milele,
mataifa wataangamia watoke nchini mwake.
10:17 Za 9:12; Kut 22:23Unasikia, Ee Bwana, shauku ya wanaoonewa,
wewe huwatia moyo, na kusikiliza kilio chao,
10:18 Kum 24:17; Za 146:9; 9:9ukiwatetea yatima na walioonewa,
ili mwanadamu, ambaye ni udongo, asiogopeshe tena.