Zaburi 89:30-37 NEN

Zaburi 89:30-37

89:30 2Sam 7:14; Yer 9:13“Kama wanae wataacha amri yangu

na wasifuate sheria zangu,

kama wakihalifu maagizo yangu

na kutoshika amri zangu,

89:32 2Sam 7:14nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo,

uovu wao kwa kuwapiga,

89:33 2Sam 7:15lakini sitauondoa upendo wangu kwake,

wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.

89:34 Hes 23:19Mimi sitavunja agano langu

wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.

89:35 Za 110:4; Ebr 6:13, 17; Amo 4:2; 8:7Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu,

nami sitamdanganya Daudi:

89:36 Za 89:4; 2Sam 7:18; Lk 1:33; Yn 12:34kwamba uzao wake utaendelea milele,

na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;

89:37 Yer 31:35; 33:20, 21kitaimarishwa milele kama mwezi,

shahidi mwaminifu angani.”

Read More of Zaburi 89