Zaburi 44:13-26
44:13 2Nya 29:8; Isa 30:3; Yer 25:9; 42:18; 44:8; Kum 28:37; Mik 2:6; Za 79:4; 80:6; 89:41; Eze 23:32Umetufanya lawama kwa jirani zetu,
dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.
44:14 1Fal 9:7; 2Fal 19:21Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa,
mataifa hutikisa vichwa vyao.
44:15 Mwa 30:23; 2Nya 32:21; Za 35:26; 34:5Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa,
na uso wangu umejaa aibu tele,
44:16 Za 42:10; 10:13; 55:3; 74:10; 1Sam 18:25; Yer 11:19; Rum 12:19kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana,
kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.
44:17 Kum 6:12; 32:18; Mit 3:1; Dan 9:13; Za 119:16, 61, 153, 176Hayo yote yametutokea,
ingawa tulikuwa hatujakusahau
wala hatujaenda kinyume na agano lako.
44:18 Za 119:51, 157Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma;
nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.
44:19 2Nya 14:13; Za 51:8; Isa 43:12; Ay 30:29; 3:5Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha,
na ukatufunika kwa giza nene.
44:20 Kum 32:18; Amu 4:7; Isa 43:12; Kut 20:3; Yer 5:12Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu
au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,
44:21 1Sam 16:7; 1Fal 8:39; Yn 2:25; Mit 15:11; Yer 12:3; 17:10; Ay 31:14; Za 139:1; Mhu 12:14; Mdo 1:24; Ufu 2:23; Rum 2:16; Ebr 4:12je, Mungu hangaligundua hili,
kwa kuwa anazijua siri za moyo?
44:22 Yer 11:19; 12:3; Isa 53:7; Rum 8:36Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;
tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.
44:23 Za 7:6; 78:65; 59:5; 74:1; 77:7Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala?
Zinduka! Usitukatae milele.
44:24 Mao 5:20Kwa nini unauficha uso wako
na kusahau taabu na mateso yetu?
44:25 Za 119:25Tumeshushwa hadi mavumbini,
miili yetu imegandamana na ardhi.
44:26 Za 102:13; 26:11; 12:5; 6:4; Hes 10:25Inuka na utusaidie,
utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.