Zaburi 25:16-22
25:16 Hes 6:25; Za 6:4; 68:6Nigeukie na unihurumie,
kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka.
25:17 1Fal 1:29; Za 6:3; 39:2; 34:6, 17; 40:12; 54:7; 116:3Shida za moyo wangu zimeongezeka,
niokoe katika dhiki yangu.
25:18 Za 13:3; Rum 12:12; 2Sam 16:12Uangalie mateso na shida zangu
na uniondolee dhambi zangu zote.
25:19 Za 3:1; 9:13; 69:4; 35:19Tazama adui zangu walivyo wengi,
pia uone jinsi wanavyonichukia vikali!
25:20 Za 2:12; 86:2; 17:13; 22:21; 43:1; 71:2; 116:4; 140:1; 142:6; 144:11Uyalinde maisha yangu na uniokoe,
usiniache niaibike,
kwa maana nimekukimbilia wewe.
25:21 Mwa 20:5; Mal 2:6; Mit 10:9; 1Fal 9:4; Za 88:10; 111:8; Isa 60:17Uadilifu na uaminifu vinilinde,
kwa sababu tumaini langu ni kwako.
25:22 Za 103:8; Lk 24:21Ee Mungu, wakomboe Israeli,
katika shida zao zote!