Zaburi 114:1-8
Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
114:1 Kut 13:3; 29:46Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
114:2 Kut 15:17; Za 76:1; 78:68, 69Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
114:3 Kut 14:21; Za 77:16; Kut 15:8; Yos 3; 16Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
114:4 Amu 5:5milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
114:5 Kut 14:21Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
114:7 Kut 15:14; 1Nya 16:30Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
114:8 Kut 17:6; Hes 20:11aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.