Zaburi 106:40-48
106:40 Law 26:28; Kut 34:9; 9:29Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake
na akauchukia sana urithi wake.
106:41 Amu 2:14; Neh 9:27Akawakabidhi kwa mataifa
na adui zao wakawatawala.
106:42 Amu 4:3Adui zao wakawaonea
na kuwatia chini ya mamlaka yao.
106:43 Amu 7:1-25; 2:16-19; 6:1-7; Yos 10:14; Neh 9:28Mara nyingi aliwaokoa
lakini walikuwa wamezama kwenye uasi,
nao wakajiharibu katika dhambi zao.
106:44 Amu 3:9; 10:10Lakini akaangalia mateso yao
wakati aliposikia kilio chao;
106:45 Mwa 9:15; Lk 1:72; Za 105:8; 103:11; 17:7; Law 26:41; Mao 3:32; Kut 32:14kwa ajili yao akakumbuka agano lake,
na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
106:46 1Nya 16:8; Mt 19:17; 2Nya 5:13; 7:3Akawafanya wahurumiwe
na wote waliowashikilia mateka.
106:47 Za 147:2; 105:1; 30:4; 99:3; 28:9; 107:3; Isa 11:12; 27:13; 56:8; 66:20; Yer 31:8; Lk 1:74; Eze 20:34; Mik 4:6; 2Kor 5:15Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe.
Tukusanye tena kutoka kwa mataifa,
ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu,
na kushangilia katika sifa zako.
106:48 Za 41:13; 72:19Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli,
tangu milele na hata milele.
Watu wote na waseme, “Amen!”
Msifuni Bwana.