Zaburi 103:1-12
Zaburi 103
Upendo Wa Mungu
Zaburi ya Daudi.
103:1 Za 28:6; 104:1; 30:4Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana.
Vyote vilivyomo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
103:2 Za 106:1; 117:1; Kum 6:12; Za 77:11Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana,
wala usisahau wema wake wote,
103:3 Kut 34:7; 15:26; Kol 3:13; 1Pet 2:24; 1Yn 1:9akusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,
103:4 Za 34:22; 56:13; 8:5; 23:6; Isa 43:1aukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji ya upendo na huruma,
103:5 Ay 33:25; Za 90:14; 104:28; 119:25, 93; 2Kor 4:16; Kut 19:4atosheleza mahitaji yako kwa vitu vyema,
ili ujana wako uhuishwe kama wa tai.
103:6 Za 9:8; 74:21; 65:5; Isa 9:7; Lk 4:10Bwana hutenda haki,
naye huwapa hukumu ya haki wote wanaoonewa.
103:7 Za 99:7; 147:19; 106:22; Kut 33:13Alijulisha Mose njia zake,
na wana wa Israeli matendo yake.
103:8 Kut 22:27; 34:6; Za 86:15; Mik 7:18-19; Yak 5:11; Kum 5:10; Hes 14:18Bwana ni mwingi wa huruma na mwenye neema;
si mwepesi wa hasira, bali amejaa upendo.
103:9 Yer 3:5, 12; Mik 7:18; Isa 57:16; Za 30:5; 79:5Yeye hatalaumu siku zote,
wala haweki hasira yake milele,
103:10 Ezr 9:13; Rum 6:23yeye hatutendei kulingana na dhambi zetu
wala hatupatilizi kwa kadiri ya maovu yetu.
103:11 Efe 3:18; Za 13:5; 57:10; 100:5; 106:45; 117:2; Mao 3:22; 2Nya 6:31Kama vile mbingu zilivyo juu ya dunia sana,
ndivyo wema wake ulivyo mwingi kwa wanaomcha;
103:12 2Sam 12:13; Rum 4:7; Efe 1:7; 2:5; Isa 43:25kama mashariki ilivyo mbali na magharibi,
ndivyo Mungu alivyoziweka dhambi zetu mbali nasi.