Mithali 9:13-18
9:13 Mit 7:11; 5:6Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele;
hana adabu na hana maarifa.
9:14 Eze 16:25Huketi kwenye mlango wa nyumba yake,
juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
9:15 Mit 1:20akiita wale wapitao karibu,
waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
9:16 Mit 1:22Anawaambia wale wasio na akili,
“Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
9:17 Mit 20:17“Maji yaliyoibiwa ni matamu;
chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
9:18 Mit 2:18; 7:26-27Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo,
kwamba wageni wake huyo mwanamke
wako katika vilindi vya kuzimu.