Mithali 8:1-11 NEN

Mithali 8:1-11

Wito Wa Hekima

8:1 Mit 1:20; 9:3; Ay 28:12; 1Kor 1:24Je, hekima haitani?

Je, ufahamu hapazi sauti?

Juu ya miinuko karibu na njia,

penye njia panda, ndipo asimamapo;

8:3 Ay 29:7; Mit 7:6-13kando ya malango yaelekeayo mjini,

kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:

8:4 Isa 42:2“Ni ninyi wanaume, ninaowaita;

ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.

8:5 Mit 1:22; 1:4Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili;

ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.

8:6 Za 49:3; Mt 2:6, 7; Kol 1:26Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema;

ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.

8:7 Za 37:30; Yn 8:14; Rum 15:8Kinywa changu husema lililo kweli,

kwa maana midomo yangu huchukia uovu.

Maneno yote ya kinywa changu ni haki;

hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.

Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi;

hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.

8:10 Za 19:10; Mit 3:14-15Chagua mafundisho yangu badala ya fedha,

maarifa badala ya dhahabu safi,

8:11 Ay 28:15-19; Mit 3:13-15kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani

na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.

Read More of Mithali 8