Mithali 7:6-20
Kwenye dirisha la nyumba yangu
nilitazama nje kupitia upenyo
kwenye mwimo wa dirisha.
7:7 Mit 6:32Niliona miongoni mwa wajinga,
nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,
kijana asiye na akili.
Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,
akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
7:9 Ay 24:15wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,
giza la usiku lilipokuwa likiingia.
7:10 1Tim 2:9Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,
hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
7:11 Mit 9:13; 1Tim 5:13(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,
miguu yake haitulii nyumbani;
7:12 Mit 8:1-36; 23:26-28mara kwenye barabara za mji,
mara kwenye viwanja vikubwa,
kwenye kila pembe huvizia.)
7:13 Mwa 39:12; Mit 1:20Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,
na kwa uso usio na haya akamwambia:
7:14 Law 7:11-18“Nina sadaka za amani nyumbani;
leo nimetimiza nadhiri zangu.
Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;
nimekutafuta na nimekupata!
7:16 Isa 19:9Nimetandika kitanda changu
kwa kitani za rangi kutoka Misri.
7:17 Amo 6:4; Mwa 37:25Nimetia manukato kitanda changu
kwa manemane, udi na mdalasini.
7:18 Mwa 39:7Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;
tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
Mume wangu hayupo nyumbani;
amekwenda safari ya mbali.
Amechukua mkoba uliojazwa fedha
na hatakuwepo nyumbani karibuni.”