Mithali 7:21-27
7:21 Mit 1:8-9; 8:32Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;
alimshawishi kwa maneno yake laini.
7:22 Ay 18:10Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke
kama fahali aendaye machinjoni,
kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
7:23 Ay 15:22; 16:13; Mit 6:26; Mhu 9:12mpaka mshale umchome ini lake,
kama ndege anayenaswa kwenye mtego,
bila kujua itamgharimu maisha yake.
7:24 Mit 1:8-9; 8:32Sasa basi wanangu, nisikilizeni;
sikilizeni kwa makini nisemalo.
7:25 Mit 5:7-8Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,
wala usitangetange katika mapito yake.
7:26 Neh 13:26Aliowaangusha ni wengi;
aliowachinja ni kundi kubwa.
7:27 Amu 16:19; Ufu 22:15Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.