Mithali 7:1-5
Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi
7:1 Mt 1:8Mwanangu, shika maneno yangu
na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
7:2 Mit 4:4; Law 18:5; Kum 32:10Shika amri zangu nawe utaishi;
linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
7:3 Kum 6:8; Mit 3:3; Isa 30:8; 2Kor 3:3Yafunge katika vidole vyako;
yaandike katika kibao cha moyo wako.
Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”
uite ufahamu jamaa yako;
7:5 Ay 31:9; Mit 2:16watakuepusha na mwanamke mzinzi,
kutokana na mwanamke mpotovu
na maneno yake ya kubembeleza.