Mithali 6:30-35 NEN

Mithali 6:30-35

Watu hawamdharau mwizi kama akiiba

kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

6:31 Kut 22:1-14Pamoja na hayo, kama akikamatwa,

lazima alipe mara saba,

ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

6:32 Kut 20:14; Mit 7:7; 9:4, 16Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;

yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

6:33 Mit 5:9-14Mapigo na aibu ni fungu lake

na aibu yake haitafutika kamwe;

6:34 Hes 5:14; Mwa 34:7kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,

naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

6:35 Ay 31:9-11; Wim 8:7Hatakubali fidia yoyote;

atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

Read More of Mithali 6