Mithali 6:12-19
Mtu mbaya sana na mlaghai,
ambaye huzungukazunguka
na maneno ya upotovu,
6:13 Za 35:19; Mit 16:30ambaye anakonyeza kwa jicho lake,
anayetoa ishara kwa miguu yake
na kuashiria kwa vidole vyake,
6:14 Za 36:4; 140:2; Mik 2:1; Isa 32:7ambaye hupanga ubaya
kwa udanganyifu moyoni mwake:
daima huchochea fitina.
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;
ataangamizwa mara, pasipo msaada.
6:16 Mit 3:32; 8:13; 15:8, 9, 26; 16:5Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,
naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
6:17 Za 120:2; Mit 12:22; Yer 2:34; Mik 7:2; Hos 4:1-2macho ya kiburi,
ulimi udanganyao,
mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
6:18 Mwa 6:5; Ay 15:31; Rum 3:15moyo uwazao mipango miovu,
miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
6:19 Kum 19:16; Za 27:12; Mit 15:18; Zek 8:17shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,
na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.