Mithali 5:1-14
Onyo Dhidi Ya Uzinzi
5:1 Mit 1:8Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu,
sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,
5:2 Mwa 2:7ili uweze kutunza busara
na midomo yako ihifadhi maarifa.
5:3 Za 55:21; Mit 2:16Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba
hudondoza asali,
na maneno ya kinywa chake
ni laini kuliko mafuta;
5:4 Mhu 7:26; Ebr 4:12lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,
mkali kama upanga ukatao kuwili.
5:5 Za 9:17; Mit 2:18Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;
hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.5:5 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.
5:6 Mit 9:13; 30:20Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;
njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
5:7 Mit 1:8-9Sasa basi wanangu, nisikilizeni;
msiache ninalowaambia.
5:8 Mit 6:20-29; 7:1-27Njia zenu ziwe mbali naye,
msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine
na miaka yako kwa aliye mkatili,
5:10 Mit 29:3wageni wasije wakasherehekea utajiri wako
na jitihada yako ikatajirisha
nyumba ya mwanaume mwingine.
Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu,
wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu!
Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!
Sikuwatii walimu wangu
wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.
5:14 Mit 1:24-27; 6:33; 31:3Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa
katikati ya kusanyiko lote.”