Mithali 4:20-27
4:20 Za 34:11-16; Mit 1:8-9; 5:1Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia;
sikiliza kwa makini maneno yangu.
4:21 Mit 3:21Usiruhusu yaondoke machoni pako,
yahifadhi ndani ya moyo wako;
4:22 Mit 3:8kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata
na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
4:23 Mit 10:11; Mt 12:34Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo,
maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
Epusha kinywa chako na ukaidi;
weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
4:25 Ay 31:1Macho yako na yatazame mbele,
kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
4:26 Ebr 12:13Sawazisha mapito ya miguu yako
na njia zako zote ziwe zimethibitika.
4:27 Law 10:11; Kum 28:14Usigeuke kulia wala kushoto;
epusha mguu wako na ubaya.