Mithali 4:1-9
Hekima Ni Bora Kupita Vitu Vyote
4:1 Mit 1:8; 19:20; Ay 8:10Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu;
sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
Ninawapa mafundisho ya maana,
kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
4:3 1Nya 29:1; 2Sam 12:24Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu,
ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
4:4 Mit 7:2; 1Nya 28:9baba alinifundisha akisema,
“Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote;
yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
4:5 Mit 3:13-18; 16:16Pata hekima, pata ufahamu;
usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
4:6 2The 2:10; Mit 2:11Usimwache hekima naye atakuweka salama;
mpende, naye atakulinda.
4:7 Mt 13:44-46; Mit 23:23Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima.
Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
4:8 1Sam 2:30; Mit 3:18Mstahi, naye atakukweza;
mkumbatie, naye atakuheshimu.
4:9 Mit 1:8-9Atakuvika shada la neema kichwani mwako
na kukupa taji ya utukufu.”