Mithali 30:11-23 NEN

Mithali 30:11-23

30:11 Mit 20:20“Wako watu wale ambao huwalaani baba zao

na wala hawawabariki mama zao;

30:12 Lk 18:11; Mit 16:2; Yer 2:23-35wale ambao ni safi machoni pao wenyewe

kumbe hawakuoshwa uchafu wao;

30:13 Ay 41:34wale ambao daima macho yao ni ya kiburi,

ambao kutazama kwao ni kwa dharau;

30:14 Ay 24:9; 29:17; Za 14:4; 57:4; Amo 8:4; Mik 2:2wale ambao meno yao ni panga

na ambao mataya yao yamewekwa visu

kuwaangamiza maskini katika nchi,

na wahitaji kutoka miongoni mwa wanadamu.

30:15 Mit 27:20“Mruba anao binti wawili waliao,

‘Nipe! Nipe!’

“Kuna vitu vitatu visivyotosheka kamwe,

naam, viko vinne visivyosema, ‘Yatosha!’:

30:16 Isa 5:14; Hab 2:5Ni kaburi, tumbo lisilozaa,

nchi isiyoshiba maji kamwe,

na moto, usiosema kamwe, ‘Yatosha!’

30:17 Kum 21:18-21; Mit 20:20; Law 20:9; Ay 15:23“Jicho lile limdhihakilo baba,

lile linalodharau kumtii mama,

litangʼolewa na kunguru wa bondeni,

litaliwa na tai.

“Kuna vitu vitatu vinavyonishangaza sana,

naam, vinne nisivyovielewa:

Ni mwendo wa tai katika anga,

mwendo wa nyoka juu ya mwamba,

mwendo wa meli katika maji makuu ya bahari,

nao mwendo wa mtu pamoja na msichana.

30:20 Mit 5:6“Huu ndio mwendo wa mwanamke mzinzi,

hula akapangusa kinywa chake na kusema,

‘Sikufanya chochote kibaya.’

“Kwa mambo matatu nchi hutetemeka,

naam, kwa mambo manne haiwezi kuvumilia:

30:22 Mit 19:10; 29:2; Mhu 10:7Mtumwa awapo mfalme,

mpumbavu ashibapo chakula,

mwanamke asiyependwa aolewapo,

naye mtumishi wa kike achukuapo nafasi ya bibi yake.

Read More of Mithali 30