Mithali 3:21-35
3:21 Mit 1:8-9; 6:20; 4:20-22Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara,
usiache vitoke machoni pako;
3:22 Kum 30:20; Mit 4:20-22ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako
na pambo la neema shingoni mwako.
Kisha utaenda katika njia yako salama,
wala mguu wako hautajikwaa;
3:24 Law 26:6; Za 3:5; Ay 11:18; Yer 31:25ulalapo, hautaogopa;
ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
3:25 Za 91:5; 112:7Usiogope maafa ya ghafula
au maangamizi yanayowapata waovu,
3:26 1Sam 2:9kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako
na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
3:27 Rum 13:7; Gal 6:10Usizuie wema kwa wale wanaostahili
ikiwa katika uwezo wako kutenda.
3:28 Law 19:13; Lk 10:25-37; Kum 24:15Usimwambie jirani yako,
“Njoo baadaye, nitakupa kesho”:
wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
3:29 Zek 8:17Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako,
ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
3:30 Rum 12:18Usimshtaki mtu bila sababu,
wakati hajakutenda dhara lolote.
3:31 Za 37:1; Mit 24:1-2Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri
wala kuchagua njia yake iwayo yote,
3:32 Za 101:4; Ay 29:4kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu,
lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
3:33 Ay 5:3; Mal 2:2; Zek 5:4Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu,
lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
3:34 Za 18:25-27; Mt 23:12Huwadhihaki wale wanaodhihaki,
lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Wenye hekima hurithi heshima,
bali huwaaibisha wapumbavu.