Mithali 3:11-20
3:11 Mit 1:8-9; Ay 5:17Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana
na usichukie kukaripiwa naye,
3:12 Mit 13:24; Ufu 3:19; Ay 3:19; 5:17; Ebr 12:5-6kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao,
kama vile baba afanyavyo
kwa mwana apendezwaye naye.
3:13 Mit 8:34, 35Heri mtu yule aonaye hekima,
mtu yule apataye ufahamu,
3:14 Ay 28:15; Mit 16:16kwa maana hekima ana faida kuliko fedha
na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
3:15 Ay 28:17-19Hekima ana thamani kuliko marijani;
hakuna chochote unachokitamani
kinachoweza kulinganishwa naye.
3:16 1Fal 3:13-14; Mit 8:18Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume;
katika mkono wake wa kushoto
kuna utajiri na heshima.
3:17 Mit 16:7; Mt 11:28-30Njia zake zinapendeza,
mapito yake yote ni amani.
3:18 Mwa 2:9; Ufu 2:7Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia;
wale wamshikao watabarikiwa.
3:19 Ay 28:25-27; Za 104:24; Mit 8:27-29Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia,
kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
3:20 Kum 33:28; Ay 36:28kwa maarifa yake vilindi viligawanywa,
nayo mawingu yanadondosha umande.