Mithali 29:19-27
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu,
ajapoelewa, hataitikia.
29:20 Mit 14:17Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka?
Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani,
atamletea sikitiko mwishoni.
29:22 Mit 14:17Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi,
naye mtu mwenye hasira ya haraka
hutenda dhambi nyingi.
29:23 Isa 66:2; Mt 23:12; Yak 4:6Kiburi cha mtu humshusha,
bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu
hupata heshima.
29:24 Law 5:1Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe;
huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
29:25 1Sam 15:24; Mit 28:25; 16:20Kuwaogopa watu huwa ni mtego,
bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
29:26 Mit 19:6; 16:33Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala,
bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
29:27 Mit 29:10Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu;
waovu huwachukia sana wenye haki.