Mithali 29:1-9 NEN

Mithali 29:1-9

29:1 2Nya 36:16; Mit 6:15Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi,

ataangamia ghafula, wala hapati dawa.

29:2 2Fal 11:20; Es 8:15; Mit 28:12Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi;

waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.

29:3 1Fal 1:48; Mit 10:1; 23:15-16; 5:8-10; Lk 15:11-32Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake,

bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.

29:4 Mit 8:15-16Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti,

bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.

29:5 Ay 32:21; Mit 26:28Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili,

anautandaza wavu kuitega miguu yake.

29:6 Ay 5:13; Mhu 9:12Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe

bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.

29:7 Ay 29:16; Za 41:1; Isa 35:3-4Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini,

bali mwovu hajishughulishi na hilo.

29:8 Mit 11:11; 16:14Wenye mzaha huuchochea mji,

bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.

29:9 Mt 11:17Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu,

mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.

Read More of Mithali 29