Mithali 28:18-28 NEN

Mithali 28:18-28

28:18 Es 6:13; Mit 10:9Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama

hulindwa salama,

bali yeye ambaye njia zake ni potovu

ataanguka ghafula.

28:19 Mit 12:11Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,

bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.

28:20 Mit 13:11; 20:21; 23:4, 22; 1Tim 6:9Mtu mwaminifu atabarikiwa sana,

bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka

hataacha kuadhibiwa.

28:21 Eze 13:19; Za 94:21; Mit 18:5Kuonyesha upendeleo si vizuri,

hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.

28:22 Mit 28:20Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri,

naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.

28:23 Mit 27:5, 6Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi,

kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.

28:24 Mit 18:9; 19:26Yeye amwibiaye babaye au mamaye

na kusema, “Si kosa,”

yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.

28:25 1Tim 6:6; Mit 29:25Mtu mwenye tamaa huchochea fitina,

bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.

28:26 Za 4:5; Mit 3:5Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu,

bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.

28:27 Kum 15:7; Mit 19:17; 22:9Yeye ampaye maskini

hatapungukiwa na kitu chochote,

bali yeye awafumbiaye maskini macho

hupata laana nyingi.

28:28 Mit 28:12; Ay 20:19Wakati waovu watawalapo,

watu huenda mafichoni,

bali waovu wanapoangamia,

wenye haki hufanikiwa.

Read More of Mithali 28