Mithali 27:5-14
27:5 Gal 2:14Afadhali karipio la wazi
kuliko upendo uliofichika.
27:6 Za 141:5; Mit 28:23Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu,
bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
27:7 Ay 6:7Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali,
bali kwa mwenye njaa
hata kile kilicho kichungu
kwake ni kitamu.
27:8 Isa 16:2; Ay 39:14Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake,
ndivyo alivyo mtu atangatangaye
mbali na nyumbani mwake.
27:9 Es 2:12; Za 45:8Manukato na uvumba huleta furaha moyoni,
nao uzuri wa rafiki huchipuka
kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
27:10 Mit 17:17Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako,
tena usiende nyumbani mwa ndugu yako
wakati umepatwa na maafa.
Bora jirani wa karibu
kuliko ndugu aliye mbali.
27:11 Mit 10:1; 23:15-16; Mwa 24:60Mwanangu, uwe na hekima,
nawe ulete furaha moyoni mwangu,
ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote
anitendaye kwa dharau.
27:12 Mit 22:3Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha,
bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
27:13 Mit 20:16Chukua vazi la yule awekaye dhamana
kwa ajili ya mgeni;
lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo
kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
27:14 Za 12:2Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu
asubuhi na mapema,
itahesabiwa kama ni laana.