Mithali 26:3-12
26:3 Za 32:9; Mit 10:13Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,
nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
26:4 Isa 36:21Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
26:5 Mt 16:14; 21:24-27; Mit 3:7Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
26:6 Mit 10:26Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara,
ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
26:7 Mit 26:9Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia
ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
26:8 Mit 26:1Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,
ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
26:9 Mit 26:7Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi
ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo,
ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
26:11 Kut 8:15; Za 85:8; 2Pet 2:22Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake,
ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
26:12 Ufu 3:17; Mit 29:20Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima
machoni pake mwenyewe?
Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.