Mithali 25:1-10
Mithali Zaidi Za Solomoni
25:1 1Fal 4:32Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
25:2 Kum 29:29; Rum 11:33; Mit 10:10-15Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo,
bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini,
ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
25:4 2Tim 2:21Ondoa takataka kwenye madini ya fedha,
nako ndani yake kutatokea chombo
cha mfua fedha.
25:5 2Sam 7:13; Mit 20:8; 29:14Ondoa waovu mbele ya mfalme,
nacho kiti chake cha enzi
kitaimarishwa kwa njia ya haki.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme,
wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
25:7 Lk 14:7-10ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,”
kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu.
Kile ulichokiona kwa macho yako
25:8 Mit 17:14; Mt 5:25-26usiharakishe kukipeleka mahakamani,
maana utafanya nini mwishoni
kama jirani yako atakuaibisha?
25:9 Mt 5:25; 18:15Kama ukifanya shauri na jirani yako,
usisaliti siri ya mtu mwingine,
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha
na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.