Mithali 24:5-14 NEN

Mithali 24:5-14

24:5 Mit 21:22Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa,

naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,

24:6 Mit 11:14; Lk 14:31kwa kufanya vita unahitaji uongozi

na kwa ushindi washauri wengi.

24:7 Za 10:5; Mit 14:6Hekima i juu mno kwa mpumbavu,

katika kusanyiko langoni

hana lolote la kusema.

24:8 Rum 1:30Yeye apangaye mabaya

atajulikana kama mtu wa hila.

24:9 Mwa 6:5; Za 119:113; Mt 9:4; Mdo 8:22; 2Kor 10:524:9 Mwa 6:5; Mdo 8:22; 2Kor 10:5Mipango ya upumbavu ni dhambi,

watu huchukizwa na mwenye dhihaka.

24:10 Yer 51:46; Ebr 12:3Ukikata tamaa wakati wa taabu,

jinsi gani nguvu zako ni kidogo!

24:11 Isa 58:6-7; 1Yn 3:16; Za 82:4Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo;

wazuie wote wanaojikokota

kuelekea machinjoni.

24:12 Za 139:2; Mit 16:24; 21:2; Yer 32:19; Mt 16:24Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,”

je, yule apimaye mioyo halitambui hili?

Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili?

Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?

24:13 Wim 5:1Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri;

asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.

24:14 Za 119:103; Mit 16:24; 23:18Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako,

kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo,

nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.

Read More of Mithali 24