Mithali 24:15-22
24:15 Za 10:9, 10Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia
makao ya mwenye haki,
wala usiyavamie makazi yake,
24:16 Ay 5:19; Mik 7:8; Za 34:19Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena,
lakini waovu huangushwa chini na maafa.
24:17 Oba 1:12; Ay 31:29Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo;
wakati ajikwaapo,
usiruhusu moyo wako ushangilie.
24:18 Ay 31:29Bwana asije akaona na kuchukia
akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
24:19 Za 37:1Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya
wala usiwaonee wivu waovu,
24:20 Ay 18:5; Mit 13:9; Isa 3:11kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo,
nayo taa ya waovu itazimwa.
24:21 Rum 13:1-7; 1Pet 2:17Mwanangu, mche Bwana na mfalme,
wala usijiunge na waasi,
24:22 Za 73:19kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao,
naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?