Mithali 23:19-28
23:19 Kum 4:9; Mit 28:7Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima,
weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.
23:20 Hab 2:15; Rum 13:13; Isa 5:22Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo,
au wale walao nyama kwa pupa,
23:21 Mit 21:17; 19:23; 19:15kwa maana walevi na walafi huwa maskini,
nako kusinzia huwavika matambara.
23:22 Law 19:32; Efe 6:1-2Msikilize baba yako, aliyekuzaa,
wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.
23:23 Mit 4:7; 17:16; Mt 13:44Nunua kweli wala usiiuze,
pata hekima, adabu na ufahamu.
23:24 Mit 23:15-16; 10:1; 15:20Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa,
naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.
23:25 Mit 10:1Baba yako na mama yako na wafurahi,
mama aliyekuzaa na ashangilie!
23:26 Mit 5:1-6; Za 18:21Mwanangu, nipe moyo wako,
macho yako na yafuate njia zangu,
23:27 Mit 22:14kwa maana kahaba ni shimo refu
na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.
23:28 Mit 7:11-12; Mhu 7:26Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia,
naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.