Mithali 23:10-18
23:10 Kum 19:14; Mit 22:28Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani
wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,
23:11 Ay 19:25; Kut 22:22-24; Yer 50:34; Mit 15:25kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu,
atalichukua shauri lao dhidi yako.
23:12 Mit 2:2Elekeza moyo wako kwenye mafundisho
na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
23:13 Mit 13:24; 19:18; 22:18; 22:15; 29:15, 16Usimnyime mtoto adhabu,
ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.
23:14 Mit 13:24; 19:18Mwadhibu kwa fimbo
na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini.23:14 Mautini maana yake ni Kuzimu.
23:15 Mit 23:24, 25; 29:3Mwanangu, kama moyo wako una hekima,
basi moyo wangu utafurahi,
23:16 Mit 23:24utu wangu wa ndani utafurahi,
wakati midomo yako
itakapozungumza lililo sawa.
23:17 Za 73:3; Mit 28:14Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi,
bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.
23:18 Za 37:1-4; Mit 24:14-20Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako,
nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.