Mithali 21:5-16
21:5 Mit 10:4Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida,
kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
21:6 Mit 10:2; 2Pet 2:3Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo
ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
21:7 Mit 11:5Jeuri ya waovu itawaburuta mbali,
kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
21:8 Mit 2:15Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu,
bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
21:9 Mit 21:19; 19:13; 25:24Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba,
kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
21:10 Yak 4:5Mtu mwovu hutamani sana ubaya,
jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
21:11 Mit 19:25Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa,
mjinga hupata hekima;
wakati mtu mwenye hekima afundishwapo,
hupata maarifa.
21:12 1Kor 10:10; Rum 2:8; Mit 14:11Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu,
naye atawaangamiza waovu.
21:13 Ay 29:12; Zek 7:11; Mdo 7:57; Yak 2:13Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini,
yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
21:14 Mwa 32:20; Mit 18:16Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira
na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
21:15 Mit 21:9Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki,
bali kitisho kwa watenda mabaya.
21:16 Za 49:14; Eze 18:24Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu,
hupumzika katika kundi la waliokufa.