Mithali 21:27-31, Mithali 22:1-6 NEN

Mithali 21:27-31

21:27 1Fal 14:24; Amo 5:22; Mit 15:8Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo,

si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!

21:28 Isa 29:21; Mit 19:5Shahidi wa uongo ataangamia,

bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.

21:29 Mit 14:8Mtu mwovu ana uso wa ushupavu,

bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.

21:30 Ay 12:13; Yer 9:23; 2Nya 13:12; Mdo 5:39Hakuna hekima, wala akili, wala mpango

unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.

21:31 Isa 31:1; Za 3:8Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita,

bali ushindi huwa kwa Bwana.

Read More of Mithali 21

Mithali 22:1-6

22:1 Mhu 7:1Heri kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi,

kuheshimiwa ni bora kuliko fedha au dhahabu.

22:2 Ay 31:15; Mt 5:45; Za 49:1-2Tajiri na maskini wanafanana kwa hili:

Bwana ni Muumba wao wote.

22:3 Mit 14:16; 27:12; Isa 26:20Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha,

bali mjinga huendelea mbele kama kipofu nayo ikamtesa.

22:4 Mit 15:33; 10:27; Dan 4:36Unyenyekevu na kumcha Bwana

huleta utajiri, heshima na uzima.

22:5 Mit 15:19; 1Yn 5:18Katika mapito ya waovu kuna miiba na mitego,

bali yeye ailindaye nafsi yake hukaa mbali nayo.

22:6 Efe 6:4Mfundishe mtoto njia impasayo kuiendea,

naye hataiacha hata akiwa mzee.

Read More of Mithali 22