Mithali 21:17-26
21:17 Mit 23:20-21, 29-35Mtu apendaye anasa atakuwa maskini,
yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
21:18 Isa 43:3-4; Mit 11:8Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki,
nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
21:19 Mit 21:9Ni afadhali kuishi jangwani
kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
21:20 Za 112:3; Mit 10:22; Mt 25:3Katika nyumba ya mwenye hekima
kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta,
lakini mtu mpumbavu
hutafuna vyote alivyo navyo.
21:21 1Kor 15:58; Za 25:13; Mt 5:6Yeye afuatiaye haki na upendo
hupata uzima, mafanikio na heshima.
21:22 Mit 8:14; Mhu 9:15-16Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu,
na kuangusha ngome wanazozitegemea.
21:23 Za 34:13; Yak 3:2; Mit 12:13Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake
hujilinda na maafa.
21:24 Yer 43:2Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake;
hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
21:25 Mit 13:4Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake,
kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
21:26 Law 25:35; Mt 5:42Mchana kutwa hutamani zaidi,
lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.