Mithali 20:25-30, Mithali 21:1-4 NEN

Mithali 20:25-30

20:25 Mhu 5:2-5; Yer 44:25Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka

na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.

20:26 Mit 20:8Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu,

hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.

20:27 Za 119:105; Mit 16:2Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu,

huchunguza utu wake wa ndani.

20:28 Mit 29:14; Isa 16:5Upendo na uaminifu humweka mfalme salama,

kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.

20:29 Mit 16:31Utukufu wa vijana ni nguvu zao,

mvi ni fahari ya uzee.

20:30 Za 51:2; Mit 22:15Mapigo na majeraha huusafisha ubaya,

nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

Read More of Mithali 20

Mithali 21:1-4

21:1 Es 5:1; Yer 39:11-12Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana;

huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.

21:2 Mit 24:12; Lk 16:15; Yer 17:10; 1Sam 16:7Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake,

bali Bwana huupima moyo.

21:3 Hos 6:6; Mik 6:6-8Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika

zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.

21:4 Ay 41:34; Mit 6:17Macho ya kudharau na moyo wa kiburi,

ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!

Read More of Mithali 21