Mithali 20:15-24
20:15 Ay 28:12, 16, 17, 18, 19Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi,
lakini midomo inenayo maarifa
ni kito cha thamani kilicho adimu.
20:16 Kut 22:26; Mit 27:13Chukua vazi la yule awekaye dhamana
kwa ajili ya mgeni;
lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo
kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu,
bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
20:18 Mit 11:14; 24:6Fanya mipango kwa kutafuta mashauri,
ukipigana vita, tafuta maelekezo.
20:19 Mit 11:13Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika,
kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20:20 Kut 21:17; Mit 30:11; Ay 18:5; Law 20:9Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake,
taa yake itazimwa katika giza nene.
20:21 Mit 28:8; Hab 2:6Urithi upatikanao haraka mwanzoni,
hautabarikiwa mwishoni.
20:22 Mit 24:29; Yer 42:11; Kum 32:35; Rum 12:17-19Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!”
Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
20:23 Kum 25:13Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu,
nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
20:24 Mit 19:21; Yer 10:23; Rum 8:26Hatua za mtu huongozwa na Bwana.
Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?