Mithali 2:1-11
Faida Za Hekima
2:1 Mit 1:8Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu
na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,
2:2 Mit 22:17kutega sikio lako kwenye hekima
na kuweka moyo wako katika ufahamu,
2:3 Yak 1:5na kama ukiita busara
na kuita kwa sauti ufahamu,
2:4 Ay 3:21; Mt 13:44; 6:19-21na kama utaitafuta kama fedha
na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,
2:5 Kum 4:6ndipo utakapoelewa kumcha Bwana
na kupata maarifa ya Mungu.
2:6 Ay 12:13; Lk 21:15; Yak 1:5Kwa maana Bwana hutoa hekima,
na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.
2:7 Mwa 6:9; 15:1; Mit 30:5-6; Za 84:11Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,
yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,
2:8 1Sam 2:9; Za 18:25kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki
na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.
2:9 Kum 1:16Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki
na sawa: yaani kila njia nzuri.
2:10 Mit 14:33Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,
nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.
2:11 Mit 4:6Busara itakuhifadhi
na ufahamu utakulinda.