Mithali 19:3-12 NEN

Mithali 19:3-12

19:3 Mit 14:1; 9:13; 24:9; Isa 32:6; Yak 1:13-15Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake

hata hivyo moyo wake humkasirikia Bwana.

19:4 Mit 19:7; 14:20Mali huleta marafiki wengi,

bali rafiki wa mtu maskini humwacha.

19:5 Kut 23:1; Kum 19:19; Mit 1:28Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,

naye amwagaye uongo hataachwa huru.

19:6 Mit 29:26; 17:8; 18:16Wengi hujipendekeza kwa mtawala

na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.

19:7 Mit 10:15Mtu maskini huepukwa na ndugu zake wote:

Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani!

Ingawa huwafuata kwa kuwasihi,

hawapatikani popote.

19:8 Mit 16:20Yeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe,

yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.

19:9 Kum 19:19Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa,

naye amwagaye uongo ataangamia.

19:10 Mit 26:1; 30:21-23; Mhu 10:5-7Haistahili mpumbavu kuishi katika anasa,

itakuwa vibaya kiasi gani

kwa mtumwa kuwatawala wakuu.

19:11 2Fal 5:12; Mit 16:32; Mt 25:21; Efe 4:32Hekima ya mtu humpa uvumilivu,

ni kwa utukufu wake kusamehe makosa.

19:12 Za 33:3; 72:5-6; Es 1:12Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba,

bali wema wake ni kama umande juu ya nyasi.

Read More of Mithali 19