Mithali 19:23-29, Mithali 20:1-4 NEN

Mithali 19:23-29

19:23 Za 25:13; 1Tim 4:8; Ay 4:7; Mit 10:27Kumcha Bwana huongoza kwenye uzima,

kisha mtu hupumzika akiwa ameridhika,

bila kuguswa na shida.

19:24 Mit 26:15Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani,

lakini hawezi hata kuupeleka kwenye kinywa chake!

19:25 Za 141:5; Mit 9:9; 21:11Mpige mwenye mzaha, naye mjinga atajifunza busara,

mkemee mwenye ufahamu naye atapata maarifa.

19:26 Mit 28:24Yeye amwibiaye baba yake na kumfukuza mama yake

ni mwana aletaye aibu na fedheha.

19:27 Mt 7:15; Mk 4:24; Efe 4:14Mwanangu, ukiacha kusikiliza mafundisho,

utatangatanga mbali na maneno ya maarifa.

19:28 Ay 15:16Shahidi mla rushwa hudhihaki hukumu

na kinywa cha mtu mwovu humeza ubaya kwa upesi.

19:29 Kum 25:2; Mit 26:3Adhabu zimeandaliwa kwa ajili ya wenye dhihaka

na mapigo kwa ajili ya migongo ya wapumbavu.

Read More of Mithali 19

Mithali 20:1-4

20:1 Law 10:9; Hab 2:5; 1Sam 25:36; 1Fal 20:16; Mit 31:4Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi;

yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.

20:2 Mit 8:36; 19:12; Es 7:7Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba;

yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.

20:3 Mwa 13:8; Mit 17:14Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi,

bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

20:4 Mit 6:6; Mhu 10:18Mvivu halimi kwa majira;

kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama

lakini hapati chochote.

Read More of Mithali 20