Mithali 19:13-22
19:13 Mit 10:1; Es 1:18; Mit 21:9Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye,
naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha.
19:14 2Kor 12:14; Mit 18:22Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa wazazi,
bali mke mwenye busara hutoka kwa Bwana.
19:15 Mit 10:4; 20:13Uvivu huleta usingizi mzito,
naye mtu mzembe huona njaa.
19:16 Mit 16:17; Lk 10:28; Rum 2:7Yeye ambaye hutii mafundisho huulinda uhai wake,
bali yeye anayezidharau njia zake atakufa.
19:17 Kum 24:19; Mt 10:42; 2Kor 9:6Yeye amhurumiaye maskini humkopesha Bwana,
naye atamtuza kwa aliyotenda.
19:18 Mit 13:24; 23:13-14Mrudi mwanao, kwa maana katika hiyo kuna tumaini,
usiwe mshirika katika mauti yake.
Mtu mwenye kukasirika haraka ni lazima atapata adhabu yake,
kama utamwokoa, itakubidi kufanya hivyo tena.
19:20 Mit 4:1; 12:15Sikiliza mashauri na ukubali mafundisho,
nawe mwishoni utakuwa na hekima.
19:21 Es 9:25; Mhu 7:29; Yer 4:29; Mao 3:37; Ebr 6:17Kuna mipango mingi ndani ya moyo wa mtu,
lakini kusudi la Bwana ndilo litakalosimama.
Lile mtu alionealo shauku ni upendo usio na mwisho,
afadhali kuwa maskini kuliko kuwa mwongo.