Mithali 18:7-16 NEN

Mithali 18:7-16

18:7 Za 140:9; 64:8; Mhu 10:12Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake

na midomo yake ni mtego kwa nafsi yake.

18:8 Mit 26:22Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu;

huingia sehemu za ndani sana za mtu.

18:9 Mit 28:24Mtu aliye mlegevu katika kazi yake

ni ndugu na yule anayeharibu.

18:10 2Sam 22:3; Za 61:3; 18:2Jina la Bwana ni ngome imara,

wenye haki huikimbilia na kuwa salama.

18:11 Mit 10:15Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome,

wanaudhania kuwa ukuta usioweza kurukwa.

18:12 Mit 11:2; 15:33Kabla ya anguko moyo wa mtu hujaa kiburi,

bali unyenyekevu hutangulia heshima.

18:13 Mit 20:25; Yn 7:51Yeye ajibuye kabla ya kusikiliza,

huo ni upumbavu wake na aibu yake.

18:14 Mit 15:13; 17:22Roho ya mtu itastahimili katika ugonjwa

bali roho iliyovunjika ni nani awezaye kuistahimili?

18:15 Mit 15:14; Efe 1:17Moyo wa mwenye ufahamu hujipatia maarifa,

masikio ya mwenye hekima huyatafuta maarifa.

18:16 Mwa 32:20; 39:2-6; 41:38-44; 1Sam 10:4Zawadi humfungulia njia mtoaji,

nayo humleta mbele ya wakuu.

Read More of Mithali 18