Mithali 18:17-24, Mithali 19:1-2 NEN

Mithali 18:17-24

Yeye aliye wa kwanza kuleta mashtaka huonekana sahihi,

hadi mwingine ajitokezapo na kumuuliza maswali.

Kupiga kura hukomesha mashindano

na kutenganisha wapinzani wakuu wanaopingana.

18:19 1Sam 17:28Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika

kuliko mji uliozungushiwa ngome,

nayo mabishano ni kama malango

ya ngome yenye makomeo.

18:20 Mit 12:14Tumbo la mtu litajaa kutokana na tunda la kinywa chake,

atashibishwa mavuno yanayotokana na midomo yake.

18:21 Mit 13:2-3; Mt 12:37Mauti na uzima viko katika uwezo wa ulimi,

nao waupendao watakula matunda yake.

18:22 Mit 12:4; 31:10; Ay 33:26Apataye mke apata kitu chema

naye ajipatia kibali kwa Bwana.

18:23 Mwa 42:13-16; Yak 2:3Mtu maskini huomba kuhurumiwa

bali tajiri hujibu kwa ukali.

18:24 1Sam 20:42; Yn 15:13-15Mtu mwenye marafiki wengi wanaweza kumharibu,

bali yuko rafiki aambatanaye na mtu kwa karibu kuliko ndugu.

Read More of Mithali 18

Mithali 19:1-2

19:1 Mit 28:6Afadhali mtu maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama,

kuliko mpumbavu ambaye midomo yake imepotoka.

19:2 Hos 4:6; Yn 16:3; Rum 10:2Sio vizuri kuwa na juhudi bila maarifa,

wala kufanya haraka na kuikosa njia.

Read More of Mithali 19