Mithali 17:5-14
17:5 Mit 14:31; Ay 31:39; Eze 25:3; Oba 1:12Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake;
yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
17:6 Za 125:5; Mit 13:22Wana wa wana ni taji la wazee,
nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
17:7 Mit 16:10Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu:
je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
17:8 Mwa 39:21; Dan 6:3Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho;
kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
17:9 Mit 10:12; 16:28Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo,
bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua
kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu;
mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
17:12 1Sam 25:25Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,
kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
17:13 Yer 18:20; 1Sam 19:4; Rum 12:17; Za 109:4-5Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema,
kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
17:14 Mit 20:3; Mt 5:25-26; Mdo 6:1Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji;
kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.