Mithali 17:25-28, Mithali 18:1-6 NEN

Mithali 17:25-28

17:25 Mit 10:1Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake

na uchungu kwa yeye aliyemzaa.

17:26 Za 94:21; Mit 18:5Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia,

au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.

17:27 Ay 6:24; Mit 14:29Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia,

naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.

17:28 Ay 2:13; Mit 10:19Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza,

na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

Read More of Mithali 17

Mithali 18:1-6

Mtu ajitengaye na wengine

hufuata matakwa yake mwenyewe;

hupiga vita kila shauri jema.

18:2 Mit 12:23Mpumbavu hafurahii ufahamu,

bali hufurahia kutangaza

maoni yake mwenyewe.

Wakati uovu unapokuja, dharau huja pia,

pamoja na aibu huja lawama.

18:4 Za 18:16Maneno ya kinywa cha mwanadamu ni kina cha maji,

bali chemchemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.

18:5 Law 19:15; Mit 28:21; Za 82:2; Ay 13:7-8Sio vizuri kumpendelea mtu mwovu,

au kumnyima haki asiye na hatia.

18:6 Mit 10:14Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi

na kinywa chake hualika kipigo.

Read More of Mithali 18