Mithali 16:8-17 NEN

Mithali 16:8-17

16:8 Za 37:16; Mit 15:16; 17:1; Mhu 4:6Afadhali kitu kidogo pamoja na haki

kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.

16:9 Yer 10:23Moyo wa mtu huifikiri njia yake,

bali Bwana huelekeza hatua zake.

16:10 Mit 17:7Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu,

wala kinywa chake hakipotoshi haki.

16:11 Law 19:36; Mit 11:1; Eze 45:10Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana;

mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.

16:12 Mit 26:28; 25:5; 29:14; 31:5Wafalme huchukia sana kutenda maovu,

kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.

16:13 Mit 22:11Wafalme hufurahia midomo ya uaminifu;

humthamini mtu asemaye kweli.

16:14 Mwa 40:2; Ay 29:24Ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa mauti,

bali mtu mwenye hekima ataituliza.

16:15 2Nya 36:16; Mit 29:1; Yer 19:1116:15 Mwa 40:2; Ay 29:24; Mit 19:12; 25:2-7Uso wa mfalme ungʼaapo, inamaanisha uhai;

upendeleo wake ni kama wingu la mvua wakati wa vuli.

16:16 Za 49:20; Ay 28:15; Mit 3:13-14Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu,

kuchagua ufahamu kuliko fedha!

16:17 Mit 4:24-27; Isa 35:8; Mdo 24:16Njia kuu ya wanyofu huepuka ubaya;

yeye aichungaye njia yake, huchunga maisha yake.

Read More of Mithali 16